NYIMBO ZA TAARAB (HUZUNI) KATIKA ZANZIBAR, MWIMBAJI

Loading...
Thumbnail Image
Date
2019-09-19
Journal Title
Journal ISSN
Volume Title
Publisher
جامعة سبها
Abstract
Ni dhahiri kuwa, katika maendeleo ya muziki wa taarab hivi sasa, nyimbo za huzuni nazo zimeibuka kila pembe mithili ya uyoga. Hali hii ya nyimbo za furaha na huzuni zimekuwa ni sehemu ya maisha ya mwanadamu. Ongezeko hili la nyimbo za huzuni katika tasnia ya muziki wa taarab haliendani kabisa na dhamira na lengo halisi na asilia la uanzishwaji wa muziki wa taarab. Wakati huo ni kwasababu muziki kwa watawala ndani ya kasiri ya taarab, ulikusudiwa kuwapa furaha na starehe tabaka tawala ikiwa ni sehemu ya burudani wakati wa mapumziko. Haikutarajiwa Sultan awe na huzuni, kwani hupewa kila atakacho. Taarab baada ya kuwa muziki wa makabwela, tanzia na huzuni, haziachi kuwepo katika maisha yao halisi.
Description
Keywords
Citation